LCB
Kazi ya kutafuta kazi
back

Kazi ya kutafuta kazi

18.01.21Fatma Shafii

Binafsi naamini Kenya ina wenyewe na sio ya kila mtu. Maonevu na mapendeleo nilioyaona hayanipi haki ya kusema kuwa Kenya ni yangu pia. Uchumi wa Kenya ni ule wa maskini kuzidi kuwa maskini na tajiri kuzidi kutajirika.

Ni miaka minne sasa tangu nilipohitimu shahada na bado sijafanikiwa kupata kazi. Na sio ati nimezembea na makaratasi yangu ya elimu, hapana! Nimetuma ombi langu la kazi kwa kampuni zisizopungua mia tano hadi sasa. Zengine nikirejelea kila mwaka. Kupata kazi Kenya kwa wengi wetu imekuwa kama kutafuta maji jangwani. Kazi niliyoipata tangu kumaliza shule ni hiyo kutafuta kazi.

Ni jambo la kufisha moyo sana, ukizingatia wengi wetu tumesoma kwa shida. Shida ya pesa, kufikia wazazi wetu kuuza kila akiba yao ili nasi tuelimike tuweze kujismamia kimaisha katika umri huu. Walakin, tumesalia kubaki majumbani mwetu bado tukiwa na tamaa ya kupata kazi.

Nimedanganywa, nikatapeliwa na nikaibiwa yote haya kwaajili ya kupata kazi. Watu wanaajiriana wao kwa wao. Iwapo humjui yeyote kwenye nyanja za juu basi elimu yako ni sawia na kaka la yai. Mda mwengine hukaa nikawaza, je, ningepewa hela zote zile nilizofunzwa nazo nikajifungulia biashara pale awali, ningekuwa nimefika wapi saa hii? Au hata kujifunza kazi za mikono ambazo zingeniwezesha kujismamia walau kwa kiasi flani. Sio kama kuzunguka na makaratasi yangu kila uchao nikitaka niandikwe kazi afisini.

Hivi ni jambo gani lililowazuia walimu kutuelezea uhalisia wa mambo huku nje? Wangelitueleza tu kuwa kama uwezekano wa kupata kazi pindi tu unapomaliza shule basi upo na uwezekano wa kukaa bila kufanikiwa kupata kazi miaka na miaka. Kufikia saa hii, mimi hutumiwa kama mfano na wazazi wanaoshindana pindi wanapoambiwa wawakazaniye watoto wao kusoma. Wengi husema, ‘Fatma huyo, amesoma hadi chuo kikuu, amefika wapi? Amebaki kuzurura barabarani na mabahasaha kila siku kama mwendawazimu’. Inauma sana, baada ya juhudi zote nilizotia, nahisi ni kama zimeambulia patupu.

Ukosefu wa kazi umenifanya niwe depressed miaka nenda miaka rudi. Kwenye dau hili, wapo walioshindwa kustahamili na kuzama kwenye bahari ya papa na papaupanga. Wakakosa dira ya maisha, wengine wakatokea kuwa wahalifu, wengine waraibu wa dawa za kulevya, na wengi hufikia kujiua.

Naam, njia moja isipofana basi ya pili huwa walakin sio hapa Kenya. Kwani nimejaribu kwa udi na uvumba kutafuta wafadhili watakaoniwezesha kuanzisha japo kibiashara Sio jambo rahisi kama nilivyodhania. Serikali wanatangaza utoaji wa kazi na pesa za kuanzisha biashara ila zinawafikia wanaowataka wao tu. Sio kila mtu, sio kila mwenye haja.

Swali langu ni, je ninavyozidi kusukuma siku za kuzurura barabarani, hali itakuwa bora au itazidi kuzoroteka? Huu ukabila, uonevu, udhalimu, utapotea au utazidi? Hichi chakula cha nchi – hongo, kitapotea au kitazidi?

Von der Arbeit, Arbeit zu finden

18.01.21Fatma Shafii

Persönlich glaube ich schon, dass Kenia etwas zu bieten hat – nur eben nicht jedem. Unrecht und Vetternwirtschaft, wie ich sie erlebt habe, geben mir nicht das Recht zu behaupten, Kenia gehöre auch mir. Kenias Wirtschaft macht die Armen ärmer und die Reichen immer reicher.

Es ist mittlerweile vier Jahre her, dass ich meinen Abschluss gemacht habe, aber ich habe es immer noch nicht geschafft, einen Job zu finden. Nicht, dass ich nur träge auf meine Ausbildungszeugnisse gestarrt hätte, nein! Bis heute habe ich Bewerbungen an mindestens 500 Unternehmen geschickt. An einige jedes Jahr neu. In Kenia Arbeit zu finden, ist für viele von uns wie nach Wasser in der Wüste zu suchen. Der Job, den ich seit meinem Uniabschluss habe, ist die Arbeitssuche.

Das ist sehr entmutigend, wenn man bedenkt, dass viele von uns nur unter großen Schwierigkeiten gelernt haben. Da ist vor allem der Geldmangel, der unsere Eltern dazu zwingt, all ihre Ersparnisse aufzulösen, damit wir eine Ausbildung erhalten, um unser Leben unserem Alter gemäß selbstbestimmt führen zu können.
Uns bleibt jedoch nichts anderes übrig, als zu Hause zu verharren, in steter Hoffnung, doch noch einen Job zu ergattern.

Ich wurde getäuscht, betrogen und beraubt – und alles nur, um Arbeit zu bekommen. Aber die Leute stellen nur ihresgleichen ein. Wenn du niemanden in den höheren Sphären kennst, nützt dir deine Bildung soviel wie eine Eierschale. Manchmal sitze ich da und denke, hey, hätte ich mir mit all dem Geld, mit dem ich unterstützt wurde, ganz von Anfang an ein Geschäft aufbauen können – wo würde ich heute stehen? Was, wenn ich einfach ein Handwerk erlernte, das es mir ermöglicht, zumindest einen gewissen Lebensstandard zu erreichen? Anstatt jeden Morgen aufs Neue mit meinen Papieren loszuziehen, um verzweifelt zu versuchen, einen Bürojob zu ergattern.

Was hat unsere Lehrer daran gehindert, uns auf die Realität da draußen vorzubereiten? Sie hätten uns auf beide Möglichkeiten vorbereiten müssen: Diejenige, gleich nach der Schule einen Job zu kriegen, und diejenige, jahrelang erfolglos auf Arbeitssuche zu sein. Bis heute muss ich als Beispiel herhalten, wenn Eltern in Streit geraten, sobald ihnen gesagt wird, sie sollen die schulische Ausbildung ihrer Kinder voranbringen. Dann höre ich immer wieder: ‚Die Fatma hier, hat es bis zur Uni geschafft, und wo steht sie jetzt? Ihr bleibt nichts übrig, als jeden Tag mit ihren Papieren durch die Straßen zu ziehen wie eine Irre!‘ Es tut so weh, alle Anstrengungen, die ich auf mich genommen habe, fühlen sich vergebens an.

Die Arbeitslosigkeit hat mich über die Jahre depressiv gemacht. Auf diesem Boot haben so manche nicht durchgehalten und sind abgesoffen. Untergegangen in einem Meer voller Haie und Schwertfische. Sie haben die Richtschnur in ihrem Leben verloren. Einige wurden zu Kriminellen, andere drogenabhängig, viele begingen Selbstmord.

Nun, wenn der eine Weg nicht zum Ziel führt, dann eben ein anderer – nur kaum hier in Kenia. Auf Biegen und Brechen habe ich versucht, Sponsoren zu finden, die es mir ermöglichen, irgendein Geschäft auf die Beine zu stellen. Das ist allerdings nicht so einfach, wie ich dachte. Die Regierung verkündet, Arbeitsplätze zu schaffen und Startkapital für Geschäftsgründungen zur Verfügung zu stellen – das kommt aber nur bei denen an, die ihnen passen. Nicht bei jedem. Nicht bei denen, die es nötig haben.

Ich frage mich, was es bringt, wenn ich weiterhin durch die Straßen ziehe: Wird sich die Situation verbessern oder weiter verschärfen? Werden Tribalismus, Ausbeutung und Ungerechtigkeit verschwinden oder zunehmen? Und was ist mit dem landesweiten Hauptnahrungsmittel, der Bestechung – wird sie je verschwinden oder wird sie sich noch weiter ausbreiten?

Übersetzung: Guido Korzonnek

The hard work of looking for a job

18.01.21Fatma Shafii

I believe Kenya belongs to her owners and not to everyone else. The spite and favouritism that I have seen denies me the right to claim that Kenya is mine too. Kenya’s economy is that of a kind whereby a poor is likely to get poorer and a rich richer.

It has been four years now since I graduated and yet I still can’t land a job. And it’s not like I have been slack and lazy glaring at my academic certificates, no! I have sent application letters to not less than five hundred companies until now. And to some other companies, each year I have repeatedly applied to them. Finding a job in Kenya for many of us has become like longing for water in desert. The only job I have found since I ended college is the same one that I do every day — going out looking for a job.

It’s a matter of heart breaking, considering that for many of us getting a degree was a nightmare. Poverty, to a stage that our parents sold all they had for us to learn, and earn, and become self-sufficient when we reach this age. However, we still remain in our family homes with high hopes that one day we may find a job.

I have been cheated, conned and all had been stolen from me in my pursuit for a job. Employers give jobs only to the people they are related to. If you have nobody who sits in the positions of authority then your education is no better than an egg shell. There are times I take a break thinking, what if I’d been handed all the money spent on educating me and would have opened a business with it since then. Where would I have reached at this moment? Or maybe, I would have used the cash for training in handcrafts suitable to help me care for myself to a certain extent at least. Not this hard work of wandering from place to place with my certificates, time and again, keeping waiting for a desk job.

What is it that refrained teachers from letting us know about reality of the outside world? They should have told us the possibilities of both, getting a job soon after graduating and waiting for years and years for one to get hired. By now, I’m being used as a case study by parents whenever they debate on getting their children to school. Most of them say, ‘There goes Fatma, she has gone through university, where is she now? Each day she keeps moving aimlessly on streets holding envelopes like a mad woman’. This is so painful, after all my efforts, all I come to reap is nothing.

Being jobless is making me depressed year after year. In this trail, several got helplessly and drowned in ocean where sharks and swordfish roam. They lost purpose in life, a couple of them turned into criminals, others drug addicts, with many taking their own lives.

Well, when one door closes another opens but not here in Kenya. Because I’ve tried by all means to get sponsors who could back me up in becoming even a petty trader. It wasn’t as easy as I had thought. The government announces support and cash for startups but they offer it to whom they favour. Not to everyone, not to all who need it.

My question is, as I keep on wandering in the streets, will the situation get better or worse? This tribalism, spite, oppression — shall it be on the rise or disappear? This ‘good things’ of the land — bribery — shall one day be vanquished or prevail?

Translation: Elias Mutani

Print

Fatma Shafii

Fatma Shafii (pen name, Fafi) is a Swahili writer based in Kenya. She likes to write about human behaviour and emerging issues affecting the continent. Her poems, fiction and non fiction have been published in various platforms including creativewritersleague.co.ke and the online literary magazine“Lolwe.” She is the founder of SHIWAKI (Shirika La Waandishi wa Kiswahili), an association of writers of the Swahili language. She is also one of the authors of “Water Birds on the Lakeshore” , the anthology of Afro Young Adult fictions, published in French, English and Kiswahili.

Fatma Shafii, Pseudonym Fafi, ist eine in Kenia lebende Schriftstellerin. Sie schreibt gern über menschliches Verhalten und neu aufkommende Probleme, die den Kontinent betreffen. Ihre Gedichte, Belletristik und Sachbücher wurden auf unterschiedlichen Plattformen veröffentlicht, darunter creativewritersleague.co.ke und das Online-Literaturmagazin »Lolwe«. Sie ist Gründerin von SHIWAKI (Shirika la Waandishi wa Kiswahili), einer Vereinigung von Schriftsteller·innen, die auf Swahili schreiben. Sie ist Mitautorin von »Water Birds on the Lakeshore«, einer Anthologie von Belletristik junger afrikanischer Autor·innen, veröffentlicht in Französisch, Englisch und Swahili.

Fatma Shafii (pen name, Fafi) is a Swahili writer based in Kenya. She likes to write about human behaviour and emerging issues affecting the continent. Her poems, fiction and non fiction have been published in various platforms including creativewritersleague.co.ke and the online literary magazine“Lolwe.” She is the founder of SHIWAKI (Shirika La Waandishi wa Kiswahili), an association of writers of the Swahili language. She is also one of the authors of “Water Birds on the Lakeshore” , the anthology of Afro Young Adult fictions, published in French, English and Kiswahili.

Toledo Logo
360